Saturday 20 March 2010

LIGI KUU: Villa 2 Wolves 2
Katika mnechi ya kwanza ya Ligi Kuu leo Jumamosi, Aston Villa wakiwa kwao Villa Park wametoka sare na Wolverhamton Wanderers kwa bao 2-2.
Sare hii imewafanya Villa wafikishe pointi 50 sawa na Manchester City walio nafasi ya 6 na wamecheza mechi moja pungufu.
Wolves wamechupa toka nafasi ya 17 hadi ya 15.
Villa ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia John Carew kwenye dakika ya 16 na Wolves wakasawazisha dakika ya 23 kwa bao la Craddock.
Katika dakika ya 38, katika hekaheka za kuokoa, James Milner akajifunga mwenyewe na kuwapa uongozi Wolves hadi dakika ya 82 ambapo John Carew alisawazisha.

No comments:

Powered By Blogger