Thursday 18 March 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Barca na Bordeaux hao Robo Fainali!!
Jana, Barcelona wakiwa nyumbani Nou Camp, waliichapa VfB Stuttgart bao 4-0 na kutinga Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI kwa jumla ya bao 5-1.
Katika mechi nyingine, Bordeaux walishinda 2-1 dhidi ya Olympiakos na hivyo
kuingia Robo Fainali kwa jumla ya bao 3-1.
Mechi za jana zimekamilisha Timu 8 zitakazocheza Robo Fainali ambazo zitachezwa Machi 30 na 31 kwa mechi za kwanza na marudio ni Aprili 6 na 7.
Droo ya kupanga mechi za Robo Fainali itafanyika kesho.
Timu zilizo Robo Fainali:
-Arsenal
-Bayern Munich
-Manchester United
-Lyon
-Inter Milan
-CSKA Moscow
-Barcelona
-Bordeaux
LEO EUROPA LIGI: Nani kutinga Robo Fainali?
Leo usiku ni mechi za marudio za EUROPA LIGI zitakazoamua Timu 8 zitakazofuzu kuingia Robo Fainali huku wawakilishi wa England, Liverpool na Fulham, wakiwa na kibarua kigumu baada ya kufungwa ugenini mechi zao za kwanza.
Liverpool wako Anfield kurudiana na Lille ya Ufaransa baada ya kupigwa 1-0.
Fulham wako kwao Craven Cottage kucheza na Vigogo wa Italia Juventus ambao walishinda 3-1.
EUROPA LIGI: Matokeo mechi za kwanza
Atletico Madrid 0 v Sporting Lisbon 0
Benfica 1 v Marseille 1
Hamburg 3 v Anderlecht 1
Juventus 3 v Fulham 1
Lille 1 v Liverpool 0
Panathinaikos 1 v Standard Liege 3
Rubin Kazan 1 v Wolfsburg 1
Valencia 1 v Werder Bremen 1
RATIBA:
Sporting Lisbon v Atletico Madrid
Marseille v Benfica
Anderlecht v Hamburg
Fulham v Juventus
Liverpool v Lille
Standard Liege v Panathinaikos
Wolfsburg v Rubin Kazan
Werder Bremen v Valencia

No comments:

Powered By Blogger