Friday 19 March 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Droo tayariiiiii!!!!!!!!!!!!
Ni rasmi: Arsenal v Barcelona & Man United v Bayern Munich!!!
Droo ya UEFA CHAMPIONS LIGI imefanyika na Manchester United na Arsenal zimetenganishwa na zitakutana tu kwenye Fainali ikiwa Timu hizo zitashinda mechi zao za Robo Fainali na Nusu Fainali.
Kwenye Robo Fainali, Arsenal watawakwaa Mabingwa Watetezi Barcelona na Mshindi wa mechi hiyo atakutana na Mshindi wa Inter Milan au CSKA Moscow kwenye Nusu Fainali.
Manchester United atacheza na Bayern Munich Robo Fainali na Mshindi atacheza na Mshindi wa mechi ya Lyon v Bordeaux kwenye Nusu Fainali.
Robo Fainali zitachezwa Machi 30 na 31 na kurudiwa Aprili 6 na 7.
Nusu Fainali zitakuwa Aprili 20 na 21 na marudiano ni Aprili 27 na 28.
Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI ni Mei 22 kwenye Uwanja wa Real Madrid Santiago Bernabeu huko Madrid, Spain.

No comments:

Powered By Blogger