Tuesday 14 September 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI:
RATIBA MECHI ZA LEO:
Jumanne, Septemba 14
KUNDI A
FC Twente v FC Internazionale Milano
SV Werder Bremen v Tottenham Hotspur FC
KUNDI B
Olympique Lyonnais v FC Schalke 04
SL Benfica v Hapoel Tel-Aviv FC
KUNDI C
Manchester United FC v Rangers FC
Bursaspor v Valencia CF
KUNDI D
FC Barcelona v Panathinaikos FC
FC Kobenhavn v FC Rubin Kazan
LIGI KUU ENGLAND: Stoke yatoka nyuma kuibwaga Villa
Jana, Stoke City wakiwa nyumbani, walikuwa nyuma kwa bao 1-0 hadi mapumziko lakini walifufuka kipindi cha pili na kuipiga Aston Villa mabao 2-1.
Villa walipata bao lao dakika ya 35 Downing akifunga kwa kichwa cha kudaivu kufuatia krosi ya Gabriel Agbonlahor.
Kwenye dakika ya 80, Kenwyne Jones alisawazisha kwa kichwa na hilo ni bao lake la kwanza kwa Stoke tangu ahamie kutoka Sunderland.
Kwenye dakika za majeruhi, dakika ya pili ya muda huo, piga ni kupiga golini kwa Villa, ilitua kwa Difenda Robert Huth aliemalizia wavuni na kuipa Stoke ushindi wake wa kwanza tangu Ligi ianze Msimu huu.

No comments:

Powered By Blogger