Tuesday 14 October 2008

KOMBE LA DUNIA: MECHI ZA MITOANO KUINGIA FAINALI AFRIKA KUSINI 2010

ULAYA:

Timu za Mataifa ya Ulaya baada ya mikikimikiki ya mechi za Jumamosi kesho tena wanajimwaga dimbani katika mechi za Makundi ya Nchi za Ulaya kuwania nafasi za kuingia Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika huko Afrika Kusini mwaka 2010.
Nchi hizi za Ulaya zimegawanywa Makundi 9 na bingwa wa kila Kundi anaingia moja kwa moja Fainali hizo.
Nchi zitakazoshika nafasi ya pili katika Makundi hayo 9 zitakachukuliwa Timu Nane Bora kugawanywa timu mbili mbili zitakazoshindana mechi za mtoano za nyumbani na ugenini ili kupata timu nyingine nne zitakazoenda Fainali.
Uingereza ambayo ipo Kundi la 6 pamoja na Croatia, Ukraine, Belarus, Kazakhstan na Andorra inaongoza Kundi hilo ikiwa na pointi 9 baada ya kushinda mechi zake tatu za kwanza ilipozifunga Andorra 2-0, Croatia 4-1 na Kazakhstan 5-1.
Uingereza kesho Jumatano watakuwa ugenini kupambana na Belarus huko mjini Minsk.

RATIBA: Jumatano, 15 Oktoba 2008

Austria v Serbia,

Belarus v England, [saa 3 na nusu usiku bongo taimu]

Belgium v Spain,

Bosnia-Herzegovina v Armenia,

Croatia v Andorra,

Czech Republic v Slovenia,

Estonia v Turkey,

Georgia v Bulgaria,

Germany v Wales,

Greece v Switzerland,

Iceland v FYR Macedonia,

Italy v Montenegro,

Latvia v Israel,

Lithuania v Faroe Islands,

Luxembourg v Moldova,

Malta v Hungary,

Northern Ireland v San Marino,

Norway v Holland,

Portugal v Albania,

Rep of Ireland v Cyprus,

Russia v Finland,

Slovakia v Poland,

MAREKANI YA KUSINI:

Timu nne za juu za Kundi hili lenye jumla ya Nchi 10 zitaingia moja kwa moja FAINALI huko AFRiKA KUSINI mwaka 2010.
Timu ya 5 itakwenda kupambana na Mshindi wa Nne Kundi la Oceania ili kupata timu moja kati ya hizo itakayoingia FAINALI.
Mpaka sasa Paraguay ndie anaeongoza akiwa na pointi 20, wa pili ni Brazil pointi 16 , watatu ni Argentina nae ana pointi 16 [kazidiwa magoli na Brazil] na wanne ni Chile pointi 13.
Timu zote zimecheza mechi 9.

RATIBA:

Jumanne 14 Oktoba 2008

Bolivia v Uruguay

Jumatano 15 Oktoba 2008

Paraguay v Peru

Chile v Argentina

Venezuela v Ecuador

Brazil v Colombia

No comments:

Powered By Blogger