Saturday 18 October 2008

MAN U WAWEKA WAPELELEZI BRAZIL KUVUMBUA VIPAJI

Mabingwa wa Ulaya na Uingereza, Manchester United, wameweka watu wawili wa kudumu huko Brazil ili kuzunguka nchi yote na kutafuta Wachezaji chipukizi wenye vipaji ili wawasajili.
Mpaka sasa Klabu hiyo Man U inao Wachezaji wanne vijana ambao ni Anderson, Mapacha Rafael na Fabio Da Silva na Rodrigo Possebon.
Meneja wa Man U Six Alex Ferguson amethibitisha kuwepo kwa wasakaji hao kwa kusema: ‘Ni nchi ambayo lazima uiangalie kwa umakini kwani siku zote inatoa wachezaji spesho wanaomudu mechi kubwa.’

BALLACK NJE WIKI TATU

Kiungo wa Chelsea, Michael Ballack, atakuwa nje ya uwanja kwa wiki tatu baada ya kufanyiwa upasuaji kwenye miguu yote miwili baada ya kusikia maumivu mara baada ya kuichezea Timu ya Taifa ya Ujerumani walipoifunga Wales bao 1-0 siku ya Jumatano kwenye mechi ya KOMBE LA DUNIA.

No comments:

Powered By Blogger