Thursday 6 August 2009

Arsenal kujua Mpinzani wake UEFA CHAMPIONS LEAGUE kesho!!!
Kesho Ijumaa mchana huko Nyon, Switzerland, Makao Makuu ya UEFA, Chama cha Soka cha Ulaya, kutafanyika dro ya kupanga Timu zipi zinakutana kwenye Raundi ya mwisho ya Mtoano wa Kombe la UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Kwenye dro hiyo kuna jumla ya Timu 20 zinazowania nafasi 10 ili kujumuika na Timu 22 kufanya jumla ya Timu 32 zitakazogawanywa Makundi Manane ya Timu 4 kila moja zitakazocheza kwa mtindo wa ligi wa mechi za nyumbani na ugenini.
Timu hizi 20 zimegawanywa Makundi mawili ya timu 10 kila moja huku Arsenal ikiwa Kundi la “sio mabingwa” ambalo lina Makapu mawili.
Kundi jingine linaitwa “mabingwa” [Hivi ni Vilabu vilivyonyakuwa Ubingwa Nchini kwao lakini Nchi hizo hazikuingizwa moja kwa moja kwenye Makundi yatayocheza kwa Ligi kwa sababu Nchi zao ziko nafasi ya chini ya Ubora HUKO Ulaya].
Arsenal yuko Kapu la kwanza lenye Timu za Arsenal, Olympique Lyonnais [Ufaransa], Sporting Lisbon [Ureno], Panathinaikos [Ugiriki] na Vfb Stuttgart [Ujerumani].
Kapu la pili ziko ACF Fiorentina [Italia], Atletico Madrid [Spain], Celtic [Scotland], Anderlecht [Ubelgiji] na Timisoara [Romania].
Timu za Kapu la Kwanza zitacheza na Mpinzani toka Timu za Kapu la Pili.
Hivyo Mpinzani wa Arsenal anaweza kuwa mmoja kati ya ACF Fiorentina [Italia], Atletico Madrid [Spain], Celtic [Scotland], Anderlecht [Ubelgiji] au Timisoara [Romania].
Kundi la “mabingwa” nalo pia limegawanywa Makapu mawili ya Timu tano kila moja na Timu ya Kapu la Kwanza itapambanishwa na Timu toka Kapu la Pili.
Kapu la Kwanza zipo Olympiacos [Ugiriki], FC Kobenhavn [Denmark], PFC Levski Sofia [Bulgaria] na Maccabi Haifa [Israel].
Kapu la Pili zipo FC Salzburg [Austria], Apoel FC [Cyprus], FK Ventspils [Latvia], Debreceni VSC [Hungary] na FC Sheriff [Marcedonia].
Mechi hizi za Raundi hii ya Mtoano zitachezwa tarehe 18 na 19 Agosti 2009 na marudiano tarehe 25 na 26 Agosti 2009.
Mechi za Kwanza za Ligi kwenye Makundi Manane ya Timu 4 kila moja zitachezwa tarehe 15 na 16 Septemba 2009.
Ligi Kuu kumpa heshima Robson
Ligi Kuu England inayoanza Jumamosi tarehe 15 Agosti 2009 imetoa maelekezo kuwa kabla ya mechi zitakazochezwa hiyo Jumamosi na siku inayofuata Jumapili kutakuwa na dakika moja ya kushangilia ikiwa ni kutoa heshima na kumbukumbu kwa Sir Bobby Robson aliefariki hivi karibuni.
Sir Bobby Robson alikuwa Meneja wa England, Newcastle na Ipswich Town na pia Klabu za PSV Eindhoven, Sporting Lisbon, Porto na Barcelona.

Mwaka 1990 aliifikisha England Nusu Fainali ya kombe la Dunia huko Italia lakini ikakosa kuingia Fainali baada ya kubwagwa kwa penalti na Ujerumani.
Mbali ya heshima hiyo ya dakika moja, Viwanja vyenye TV kubwa vimeagizwa kuonyesha mkanda maalum wa Sir Bobby Robson
.

No comments:

Powered By Blogger