Thursday 6 August 2009

MATOKEO JANA MECHI ZA MTOANO UEFA CHAMPIONS LEAGUE: [matokeo mechi ya awali kwenye mabano]
BATE 2 v FK Ventspils 1, (0-1),

Debrecen 1 v FC Levadia Tallinn 0, (1-0),
Dinamo Moscow 0 v Celtic2, (1-0),
Levski Sofia 2 v FK Baku 0, ( 0-0),
NK Maribor 0 v FC Zurich 3, (3-2),
Olympiacos 2 v Slovan Bratislava 0, ( 2-0),
Partizan Belgrade 1 v Apoel Nicosia 0, ( 0-2),
Politehnica Timisoara 0 v Shakhtar Donetsk 0, ( 2-2),
Slavia Prague 1 v FC Sheriff Tiraspol 1, (0-0),
Stabaek 0 v FC Copenhagen 0, (1-3),
Chelsea yamkera Mourinho!!
Bosi wa Inter Milan Jose Mourinho ameishambulia Klabu yake ya zamani Chelsea kwa kutia ngumu kwa yeye kumsaini Sentahafu wa Chelsea Ricardo Carvalho.
Mourinho amedai Chelsea imeongeza dau la Carvalho baada ya kugundua wao Inter Milan wanamtaka.
Mourinho ameonyesha nia ya kuwachukua Wachezaji wake wa zamani aliokuwa nao huko Ureno na Klabu ya FC Porto Deco na Carvalho ambao sasa wako Chelsea.
Lakini Mourinho ameonyeshwa kukerwa na Chelsea na ametamka: “Ni ngumu kwa sasa kumchukua Mchezaji toka Chelsea. Kila wakigundua nina nia na Mchezaji wao mambo hubadilika ghafla! Tuliambiwa Deco yuko huru kuja kwetu lakini wiki mbili baadae, walipogundua tuna nia ya kweli, dau likatoka sifuri hadi Milioni 5! Carvalho likapanda toka Milioni 5 hadi 15!”
EUROPA LEAGUE: Marudiano leo Fulham v FK Vetra
Fulham, baada ya kupata ushindi mnono wa bao 3-0 ugenini, leo wakiwa nyumbani wanarudiana tena na FK Vetra ya Lithuania uwanjani kwao Craven Cottage.
Endapo Fulham watashinda leo wataingia Raundi ya mwisho ya Mtoano ya EUROPA LEAGUE na kucheza na Timu watakayopangiwa kwenye dro hapo Ijumaa kwa mtoano kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na wakifuzu hapo ndipo watakuwa kwenye hatua ya Makundi itakayochezwa kwa mtindo wa Ligi.
Katika Raundi ijayo ya Mtoano Klabu nyingine za Ligi Kuu England zitakazojumuika na Fulham ikifuzu ni Aston Villa na Everton.
Timu hizi mbili zitaanzia Raundi hii kwa vile zilimaliza Ligi nafasi ya 5 na 6.

Fulham ilimaliza ya 7.
Kikosi cha leo Fulham kintatokana na: Stockdale, Schwarzer, Zuberbuhler, Baird, Konchesky, Hangeland, Hughes, Pantsil, Kelly, Stoor, Andranik, Seol, Zamora, Nevland, Gera, Etuhu, Murphy, Dempsey, E Johnson, A Johnson.

No comments:

Powered By Blogger