Wednesday 5 August 2009

MTOANO UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Celtic wasonga mbele, washinda ugenini 2-0!
Baada ya kuchapwa 1-0 kwao mjini Glasgow, leo Celtic wameshinda ugenini mjini Moscow, Urusi baada ya kuinyuka Dinamo Moscow bao 2-0 huku mkombozi akiwa Mchezaji wao wa Kigiriki Georgios Samaras aliepachika bao la pili dakika za majeruhi.
Samaras aliingizwa kipindi cha pili kumbadili Mchezaji Scott MaCdonald aliefunga bao la kwanza kipindi cha kwanza.
Huku mechi ikielekea kwenda muda wa nyongeza wa nusu saa na pengine penalti kama matokeo yangebaki Dinamo Moscow 0 Celtic 1, ndipo Samaras alipopachika bao la pili na kuipeleka Celtic kwenye Raundi ya mwisho ya Mtoano kabla Ligi ya Makundi kuanza.

No comments:

Powered By Blogger