Tuesday 4 August 2009

REAL NA LIVERPOOL WAKUBALIANA KWA ALONSO!!
Liverpool imethibitisha kuwa wamefikia makubaliano na Real Madrid kuhusu kuuzwa kwa Xabi Alonso.
Alonso, umri miaka 27, amekuwa akiwindwa na Real kwa muda mrefu ingawa Liverpool imekuwa ikigoma kumuuza hasa ukitilia manani Kiungo wao mwingine Mascherano nae ameeleza matakwa yake kuhama.
Liverpool, ikithibitisha kuuzwa kwa Alonso aliehamia Anfield mwaka 2004 akitokea Real Sociedad na kucheza mechi 127, imesema dau na mkataba wa uhamisho hautangazwi.

No comments:

Powered By Blogger