Tuesday 4 August 2009

Nyota wa Bondeni kucheza Fulham
Nyota wa Afrika Kusini, Kagiso Dikgacoi, amesema amekamilisha taratibu za kujiunga na Klabu ya Ligi Kuu England, Fulham.
Mchezaji huyo wa Bafana Bafana mwenye umri wa miaka 24 anaechezea Klabu ya Golden Arrows huko Bondeni kama Kiungo alipimwa afya yake wiki iliyopita baada ya kumaliza majaribio Klabuni hapo.
Kagiso Dikgacoi, alieng’ara kwenye michuano ya Kombe la Mabara iliyomalizika hivi karibuni akichezea Timu ya Taifa ya Afrika ya Kusini Bafana Bafana, amerudi kwao Afrika Kusini kwa muda mfupi kabla ya kujiunga tena na Klabu yake mpya Fulham.
MECHI ZA MTOANO LEO UEFA CHAMPIONS LEAGUE-Marudiano [magoli mechi ya kwanza kwenye mabano]
FC Twente v Sporting, (0-0)
Maccabi Haifa v FC Aktobe, (0-0),
Panathinaikos v Sparta Prague, (1-3),
Sivasspor v Anderlecht, (0-5),
HALI YA KIFEDHA KLABU ZA ENGLAND ZAITIA KIWEWE UEFA!!!
Chama cha Soka cha Ulaya, UEFA, kimeeleza wasiwasi wake kuhusu hali ya kifedha ya Klabu za Ligi Kuu England huku Katibu Mkuu wa UEFA, David Taylor, akionya kuwa kuna baadhi ya Klbu zitaangamia kwa kile alichokiita ‘kuishi nje ya uwezo wao”.
Taylor ametamka kuwa mfano bora ni ule yaliyowapata Leeds United.
Mwaka 2001 Leeds ikiwa Ligi Kuu England ilifanikiwa kucheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE lakini msimu uliofuatia walishindwa kupata nafasi ya kucheza Ulaya na hivyo kukosa mapato na Klabu ikaingia matatani na kulazimika kuwauza Wachezaji wao nyota ili kufidia mapato.

Mwaka 2003 Leeds waliponea chupuchupu kuteremshwa Daraja lakini wakaporomoka msimu uliofuata na huo ukawa mwanzo wa kuangamia.
Leeds ikadidimia zaidi na kulazimika kuuza Uwanja wao Elland Road pamoja na viwanja vya mazoezi na wakazidi kuporomoka na mpaka sasa wako Daraja la tatu chini na Klabu imetangazwa mufilisi.
Mpaka sasa Klabu ya Liverpool iliyonunuliwa na Wamarekani wawili ipo kwenye deni kubwa.

Hata Wamiliki wa Manchester United, Familia ya Glazer, wameitumbukiza Klabu hiyo iliyokuwa na mahesabu safi na kutokuwa na chembe ya deni kwenye deni ingawa wenyewe kina Glazer wanatamba hawapo hatarini.

No comments:

Powered By Blogger