Sunday 2 August 2009

KOMBE LA EMIRATES: Arsenal wabeba Kombe lao, nyumbani kwao!
Leo, Arsenal wameibandika Glasgow Rangers mabao 3-0 Uwanjani Emirates katika mashindano ya kugombea Kombe la Emirates na kubeba Kombe hilo huku magoli mawili ya kwanza yakifungwa ndani ya dakika 10 za kwanza kupitia kwa Kijana hatari Jack Wilshere dakika ya pili na Eduardo Da Silva dakika ya 10.
Jack Wilshere tena alipachika bao la 3 dakika ya 72.
Mechi hii ilitanguliwa na mechi kati ya PSG na Atletico Madrid iliyomalizika suluhu 1-1.
Katika mechi hii Madrid walipata bao la kwanza baada ya Mlinzi wa PSG Baning kutoa penalti na kutwangwa Kadi Nyekundu kwenye dakika ya 40 na penalti hiyo ikafungwa na Serigo Leonel Aguero.
PSG, wakicheza mtu 10, walisawazishi kipindi cha pili dakika ya 71 kupitia Mchezaji wa zamani wa Barcelona Ludovic Giuly.

No comments:

Powered By Blogger