Thursday 6 August 2009

UHAMISHO………kwa ufupi!!!!!!!!!
-AC Milan imemchukua Mshambuliaji wa Kidachi kutoka Real Madrid, Klaas-Jan Huntelaar, umri miaka 26, kwa mkataba wa miaka minne.
Huntelaar alijiunga na Real mwezi Januari mwaka huu na kufunga bao 8. Kabla ya hapo alikuwa Timu ya Uholanzi Ajax kwa muda wa miaka mitatu huku akifunga mabao 76 katika mechi 92 alizocheza.
-Burnley, Klabu iliyopanda Daraja kuingia Ligi Kuu England, imemchukua kwa mkopo Winga kutoka Nchi ya Ecuador, Fernando Guerrera, miaka 19, kutoka Klabu ya Independientede Valle.
-Hull City imewachukua Wachezaji wawili, kutoka Stoke City Mnigeria Seyi Olofinjana , miaka 29, na kutoka Villareal imembeba Mshambuliaji wa USA, Jozy Altidore, kwa mkopo.
-Wigan imemsaini Winga wa Chelsea, Scott Sinclair, miaka 20, kwa mkopo utakaodumu msimu mmoja. Msimu uliokwisha Sinclair alikuwa Birmingham kwa mkopo ambako aliisaidiaTimu hiyo kupanda Daraja kuingia Ligi Kuu.

No comments:

Powered By Blogger