Wednesday 5 August 2009

MADENI YAKWAMISHA KUANZA MSIMU ARGENTINA!!!
Kuanza kwa msimu mpya wa soka huko Nchini Argentina kumekwama kufuatia kwa Klabu nyingi kukumbwa na madeni.
Msimu mpya ulitakiwa uanze Agosti 14 lakini Chama cha Soka cha Argentina [AFA] kimesema Klabu nyingi hazina pesa kuwalipa Wachezaji na sasa hali ni ngumu sana.

Rais wa AFA, Julio Grondona, amesema hali inatisha na hata Ligi Daraja la Pili iliyokuwa ianze wiki iliyokwisha imesimama na wao sasa wanatafuta ufumbuzi wa tatizo hilo kubwa.
Hata hivyo Rais huyo amesema ushiriki wa Argentina kwenye mashindano na Nchi nyingine za Marekani ya Kusini, kama vile Kombe la Sudamericana, na pambano la kirafiki la Timu ya Taifa ya Argentina na Urusi hapo Agosti 12, yataendelea kama yalivyopangwa.
Hali hiyo ya ngumu kwa Klabu za Argentina imechangiwa sana na hali tata ya uchumi duniani na pia kutopanda kwa mapato toka kwenye haki za maonyesho ya mipira kwenye Televisheni.

No comments:

Powered By Blogger