Sunday 2 August 2009

KOMBE LA EMIRATES: Magoli mechi ya Arsenal na Atletico Madrid yapatikana dakika 5 za mwisho!
Jana, kwenye Uwanja wao wa Emirates, Arsenal walikumbana na Atletico Madrid ya Spain na magoli ya mechi hiyo yalipatikana dakika 5 za mwisho za mechi pale Andre Arshavin wa Arsenal alipofunga goli dakika ya 86, Atletico wakasawazisha kupitia Pacheco dakika ya 88 lakini Arshavin tena akafunga la pili dakika ya 89 na kuwapa Arsenal ushindi.
Katika mechi nyingine ya awali hapo jana Glasgow Rangers iliifunga PSG kutoka Ufaransa kwa bao moja kwa bila.
Leo ni PSG na Atletico na baadae Arsenal na Rangers.

No comments:

Powered By Blogger