Thursday 6 August 2009

Man U 2 Valencia 0
Akicheza mechi yake ya kwanza ndani ya Jezi maarufu Nambari 7, mbele ya Washabiki zaidi ya 70,000, Uwanjani Old Trafford, akishuhudiwa pia na Meneja wa England Fabio Capello, Mshambuliaji Michael Owen, aliepata nafasi zaidi ya 3 za wazi, alishindwa kupata bao.
Na ilikuwa ni juu ya Nyota Wayne Rooney na Chipukizi Tom Cleverley kupachika mabao yaliyowapa ushindi Manchester United wakicheza mechi yao ya kwanza Uwanja wa nyumbani kabla msimu mpya kuanza dhidi ya Klabu ngumu kutoka Spain Valencia iliyokuwa na Nyota kama Villa na Silva.
Akicheza pia mechi yake ya kwanza mbele ya Mashabiki wa Man U hapo Old Trafford, Mchezaji mpya Winga Luis Antonio Valencia aling’ara sana na kuwapa matumaini makubwa Washabiki hao baada ya kuwa mpishi murua wa mabao yote hayo mawili kwa kufanya kazi nzuri winga ya kulia na kutoa krosi tamu kwa wafungaji zilizowafanya Washabiki kukumbuka enzi za David Beckham.
Jumapili, ndani ya Wembley Stadium, Jijini London, Mabingwa Manchester United watajimwaga kucheza na Mabingwa wa Kombe la FA Chelsea ikiwa mechi ya “ Fungua Pazia” msimu mpya ya kugombea Ngao ya Hisani.

No comments:

Powered By Blogger