Tuesday 4 August 2009

Lescott anataka kuhama Everton
Mlinzi wa Everton Joleon Lescott ameiambia Klabu yake kuwa dhamira yake ni kuhama ingawa mpaka sasa hajatoa maombi maalum ya kutaka kuhama huku Manchester City ikimfukuzia na iko tayari kuilipa Everton Pauni Milioni 18.
Everton mpaka sasa imegoma kumuuza Lescott lakini kuna dalili kuwa huenda wakalazimika kufanya hivyo kwani imeshadhihirika kuwa wapo kwenye mazungumzo na Arsenal ili wamchukue Mlinzi Philippe Senderos ili azibe pengo la Lescott.
Lescott alijiunga na Everton mwaka 2006 kutoka Wolverhampton kwa ada ya Pauni Milioni 5.
Wenger ang’ang’ana haongezi dau kumnunua Chamakh!!!
Arsene Wenger ametoboa kuwa hayuko tayari kuongeza dau la kumnunua Mchezaji wa kutoka Morocco, Marouane Chamakh kutoka Klabu ya Bordeaux ya Ufaransa, kwa zaidi ya Pauni Milioni 5 alizotoa ofa.
Bordeaux mpaka sasa wanataka dau liongezwa huku zikitajwatajwa Pauni Milioni 15 kama ndio wanazozitaka kwa Mchezaji huyo.
Arsene Wenger ametamka: “Katika miezi mitano ijayo, endapo Chamakh hataongeza mkataba wake na Bordeaux, atakuwa huru kuongea na Klabu yeyote! Baada ya hapo Bordeaux hawatapa senti hata moja! Sina papara ya kumchukua kwa zaidi ya ofa tuliyotoa kwanza nnao Mafowadi wengine kama Walcott, Bendtner, Van Persie, Arshavin na Eduardo!”

No comments:

Powered By Blogger