Monday 7 September 2009

Ghana watinga Bondeni, Nchi ya kwanza Afrika kuingia Fainali Kombe la Dunia 2010!!!
Ghana ni Nchi ya kwanza ya Afrika kufanikiwa kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwaka 2010 baada ya kuifunga Sudan bao 2-0 mjini Accra hapo jana.
Nchi nyingine inayonyemelea kujiunga na Ghana ni Ivory Coast, ambao juzi waliikung’uta Burkina Faso 5-0, na sasa wanahitaji pointi moja tu kutinga Fainali.
Afrika kuna Makundi matano na Mshindi wa kila Kundi ndie atacheza Fainali huko Afrika Kusini wakati Timu 3 za juu kila Kundi zitacheza Kombe la Mataifa ya Afrika huko Angola mwakani.
MATOKEO KOMBE LA DUNIA:
MECHI ZA: Jumapili Septemba 6,
Togo 1 v Morocco 1
Mozambique 1 v Kenya 0
Nigeria 2 v Tunisia 2
Algeria 1 v Zambia 0
Ghana 2 v Sudan 0
Benin 1 v Mali 1

No comments:

Powered By Blogger