Monday 8 March 2010

FA CUP: Nusu Fainali yapangwa!
Droo ya Nusu Fainali ya Kombe la FA imefanyika na Mabingwa Watetezi wa Kombe hilo Chelsea wamepangwa kucheza na Aston Villa.
Katika Robo Fainali, Chelsea waliitoa Stoke City 2-0 na Aston Villa waliibwaga Reading 4-2.
Mechi nyingine ya Nusu Fainali ni mshindi kati ya Tottenham na Fulham, waliotoka sare 0-0 juzi na watarudiana Machi 24, kukutana na Portsmouth ambao ndio walikuwa Mabingwa mwaka 2008.
Portsmouth waliifunga Birmingham 2-0 kwenye Robo Fainali.
Mechi za Nusu Fainali zitachezwa Uwanja wa Wembley Jijini London kwenye wikiendi ya Aprili 10 na 11.

No comments:

Powered By Blogger