Sunday 7 March 2010

LIGI KUU: Everton 5 Hull 1
Everton wakiwa nyumbani Goodison Park wameishindilia Hull City bao 5-1 na hivyo kuzidi kuingiza kwenye balaa Hull ambayo inaelea mkiani kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Mabao ya Everton yalifungwa na Mikel Arteta bao mbili, Leighton Barnes na Landon Donovan bao moja moja na moja Hull City walijifunga wenyewe baada ya mpira kumbabatiza Richard Garcia.
FA CUP: Chelsea 2 Stoke City 0
Frank Lampard na John Terry wameifungia Chelsea bao moja kila mmoja na kuifikisha Timu yao Nusu Fainali ya Kombe la FA na hivyo kuungana na Portsmouth na Aston Villa.
Timu ya 4 itakayoingia Nusu Fainali ni ama Tottenham au Fulham ambazo jana zilitoka 0-0 na zitarudiana White Hart Lane Machi 24.

No comments:

Powered By Blogger