Monday 17 May 2010

Ballack bai bai Kombe la Dunia
Nahodha wa Ujerumani Michael Ballack hatacheza Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini zinazoanza Juni 11 baada ya kuthibitishwa enka aliyoumia kwenye Fainali ya FA Cup hapo Jumamosi Chelsea walipoifunga Portsmouth 1-0 inahitaji wiki 8 ili apone na kuanza mazoezi.
Ballack aliumizwa na Mchezaji wa Portsmouth, Kevin-Prince Boateng, ambae ni mzaliwa wa Ujerumani lakini Baba yake anatoka Ghana na yeye mwenyewe ameamua kuchezea Ghana kwenye Fainali hizo za Kombe la Dunia na ameribakiwa na FIFA kuichezea Ghana licha ya kucheza Timu za Taifa za Vijana za Ujerumani.
Kwenye Fainali hizo za Kombe la Dunia Ujerumani na Ghana wapo Kundi D pamoja na Serbia na Australia.
Ancelotti ataka kudumu Chelsea
Carlo Ancelotti anapendelea abaki Chelsea kwa muda mrefu kufuatia kuiongoza kushinda Makombe mawili kwa mpigo Msimu uliokwisha majuzi, Makombe ya Ligi Kuu na FA.
Ancelotti amesema: “Ikiwa kila Msimu utakuwa kama huu uliopita ningependa nikae miaka 10! Niko tayari kusaini Mkataba mpya!”
Mtaliana huyo ambae alikaa na AC Milan kwa miaka minane amekiri kuongoza England ni kazi rahisi mno kwani hupewa kila kitu na ushirikiano mkubwa.
Kuhusu Msimu ujao, Ancelotti amesema mpaka sasa hajajua aongeze Wachezaji gani na wa idara ipi hasa kwa vile Wachezaji majeruhi wa muda mrefu, Jose Bosingwa na Michael Essien, watarudi upya uwanjani baada ya kupona.
Pia, Ancelotti amepinga tetesi kuwa Frank Lampard yumo mbioni kuhama Chelsea na ameng’ang’ania kuwa Lampard atabaki Klabuni hapo.
Ufaransa yapunguza Kikosi cha Kombe la Dunia
Kocha wa Ufaransa Raymond Domenech amekipunguza Kikosi alichokitangaza wiki iliyopita kutoka Wachezaji 30 hadi 24 na ameahidi kutaja Timu yake ya Wachezaji 23, wanaotakiwa kuwasilishwa FIFA ifikapo Juni 1, Mei 27.
Wachezaji 6 waliopigwa panga ni Hatem Ben Arfa wa Marseille, Kipa Mickael Landreau na Beki Adil Rami, wote wa Lille, na Wachezaji watatu toka Rennes, Rod Fanni, Yann M’Vila na Jimmy Briand.
Timu hiyo inategemewa kuanza mazoezi Ufaransa kisha kwenda kupiga kambi Nchini Tunisia.
Ufaransa ipo Kundi A pamoja na Mexico, Afrika Kusini na Uruguay.
Kikosi kamili:
MAKIPA: Hugo Lloris (Lyon ), Steve Mandanda (Marseille), Cedric Carrasso (Bordeaux);
WALINZI: Eric Abidal (Barcelona), Gael Clichy, William Gallas, Bakary Sagna (Wote wa Arsenal), Patrice Evra (Manchester United ), Marc Planus (Bordeaux), Anthony Reveillere (Lyon), Sebastien Squillaci (Sevilla);
VIUNGO: Abou Diaby (Arsenal), Lassana Diarra (Real Madrid), Alou Diarra, Yoann Gourcuff (Wote toka Bordeaux), Florent Malouda (Chelsea), Franck Ribery (Bayern Munich ), Jeremy Toulalan (Lyon);
MASTRAIKA: Nicolas Anelka (Chelsea), Thierry Henry (Barcelona), Andre-Pierre Gignac (Toulouse), Sidney Govou (Lyon), Djibril Cisse (Panathinaikos), Mathieu Valbuena (Marseille).

No comments:

Powered By Blogger