FAINALI: Nini cha kuangalia Leo!!!
Stadio Santiago Bernabeau

Mfungaji Bora: Diego Milito [Argentina]
Mechi bora kwa Milito ilikuwa ni Nusu Fainali ya kwanza Inter walipoivaa Barcelona huko San Siro alipofunga bao la kwanza na kuzitengeneza bao mbili nyingine katika ushindi wa 3-1.
Milito ameshafunga bao 4 kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu huu.
Mchezaji anaeweza kuwika: Mario Balotelli [Italy]
Tineja huyu mara nyingi huonekana mapepe lakini akitulia ni Mchezaji hatari mno na mara nyingi Mourinho humwingiza toka Benchi kuchukua namba ya Samuel Eto’o au Milito.
Nguvu ya Inter: Mtu 4 za Difensi yao zenye uzoefu- Javier Zanetti, Maicon, Lucio & Walter Samuel
Bayern Munich (Mabingwa Mara 4: 1973/74, 1974/75, 1975/76 & 2000/01)

Mfungaji Bora: Ivica Olic [Croatia]
Ni mhangaikaji mkubwa uwanjani na ameshafunga bao 7 kwenye Kombe hili Msimu huu.
Mchezaji anaeweza kuwika: Arjen Robben [Udachi]
Amefunga bao 4 katika mechi zake 5 za mwisho za Kombe hili na hivyo Difensi ya Inter Milan itabidi imchunge.
Changamoto kwa Robben ni kufunga bao katika Uwanja wa Timu iliyo mkataa na kumtupa nje- Real Madrid.
Pigo kwa Bayern: Kumkosa Franck Ribbery
Ingawa Inter Milan nao watamkosa Thiago Motta aliefungiwa kama Frank Ribery lakini pengo kubwa inaelekea litakuwa kwa Bayern kwa vile Ribery ndie injini yao kubwa.
No comments:
Post a Comment