Saturday 22 May 2010

FAINALI: Nini cha kuangalia Leo!!!
Stadio Santiago Bernabeau

Inter Milan (Mabingwa Mara mbili: 1963/64 & 1964/65)
Inter Milan inaongozwa na Kocha machachari na mwenye majivuno, Jose Mourinho, ambae ameshawahi kutwaa Kombe hili akiwa na FC Porto Mwaka 2004.
Mfungaji Bora: Diego Milito [Argentina]
Mechi bora kwa Milito ilikuwa ni Nusu Fainali ya kwanza Inter walipoivaa Barcelona huko San Siro alipofunga bao la kwanza na kuzitengeneza bao mbili nyingine katika ushindi wa 3-1.
Milito ameshafunga bao 4 kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu huu.
Mchezaji anaeweza kuwika: Mario Balotelli [Italy]
Tineja huyu mara nyingi huonekana mapepe lakini akitulia ni Mchezaji hatari mno na mara nyingi Mourinho humwingiza toka Benchi kuchukua namba ya Samuel Eto’o au Milito.
Nguvu ya Inter: Mtu 4 za Difensi yao zenye uzoefu- Javier Zanetti, Maicon, Lucio & Walter Samuel
Bayern Munich (Mabingwa Mara 4: 1973/74, 1974/75, 1975/76 & 2000/01)
Bayern Munich iko chini ya Kocha toka Udachi, Louis van Gaal, ambae alikuwa Bosi wa Mourinho walipokuwa wote FC Barcellona kati ya Mwaka 1997 na 2000.
Mfungaji Bora: Ivica Olic [Croatia]
Ni mhangaikaji mkubwa uwanjani na ameshafunga bao 7 kwenye Kombe hili Msimu huu.
Mchezaji anaeweza kuwika: Arjen Robben [Udachi]
Amefunga bao 4 katika mechi zake 5 za mwisho za Kombe hili na hivyo Difensi ya Inter Milan itabidi imchunge.
Changamoto kwa Robben ni kufunga bao katika Uwanja wa Timu iliyo mkataa na kumtupa nje- Real Madrid.
Pigo kwa Bayern: Kumkosa Franck Ribbery
Ingawa Inter Milan nao watamkosa Thiago Motta aliefungiwa kama Frank Ribery lakini pengo kubwa inaelekea litakuwa kwa Bayern kwa vile Ribery ndie injini yao kubwa.

No comments:

Powered By Blogger