Thursday 20 May 2010

Spain yatangaza Mtu 23 kwa Fainali Kombe la Dunia
Kocha wa Spain Vicente del Bosque ametangaza Kikosi chake cha mwisho cha Wachezaji 23 cha Fainali za Kombe la Dunia na majina hayo yatawsilishwa FIFA.
Kila Nchi itakayocheza Fainali hizo huko Afrika Kusini kuanzia Juni 11 zimetakiwa kufikisha FIFA Vikosi vyao vya Wachezaji 23 si zaidi ya terehe 1 Juni.
Katika Kikosi hicho wapo Mastaa Cesc Fabregas, Andres Iniesta na Fernando Torres ambao wote ni majeruhi.
Pia wamo Wachezaji watatu ambao hawajawahi kuichezea Spain nao ni Kipa Victor Valdes na Pedro wa Barcelona na Javi Martinez wa Athletic Bilbao.
Spain wapo Kundi H pamoja na Uswisi, Chile na Honduras na mechi yao ya kwanza ni Mjini Durban Juni 16 watakapocheza na Uswisi.
Spain wanategemea kucheza mechi za kujipima nguvu dhidi ya Saudi Arabia, Korea Kusini na Poland kabla kwenda Afrika Kusini.
Kikosi kamili:
MAKIPA: Iker Casillas (Real Madrid), Jose Manuel 'Pepe' Reina (Liverpool), Victor Valdes (Barcelona).
WALINZI: Raul Albiol (Real Madrid), Alvaro Arbeloa (Real Madrid), Joan Capdevila (Villarreal), Carlos Marchena (Valencia), Gerard Pique (Barcelona), Carles Puyol (Barcelona), Sergio Ramos (Real Madrid).
VIUNGO: Xabier Alonso (Real Madrid), Sergio Busquets (Barcelona), Cesc Fabregas (Arsenal), Andres Iniesta (Barcelona), Javier Martinez (Athletic Bilbao), David Silva (Valencia), Xavi Hernandez (Barcelona).
MAFOWADI: Jesus Navas (Sevilla), Juan Manuel Mata (Valencia), Pedro Rodriguez (Barcelona), Fernando Llorete (Athletic Bilbao), Fernando Torres (Liverpool), David Villa (Valencia).
Sevilla yanyakua Copa del Rey
Atletico Madrid 0 Sevilla2
Jana Sevilla waliweza kuwafunga Atletico Madrid 2-0 Uwanja wa Nou Cam katika Fainali ya Kombe la Mfalme huko Spain, maarufu kama Copa del Rey.
Mabao ya Sevilla yalifungwa na Diego Capel dakika ya 5 na la pili na Jesus Navas kwenye dakika ya 90.

No comments:

Powered By Blogger