Friday 21 May 2010

Maradona amsaga na Gari Mpigapicha
Kocha wa Argentina Diego Maradona ameelezwa kuwa alimtukana Mpigapicha mara baada ya kuukanyaga mguu wake na gari lake kwa bahati mbaya wakati akienda kutangaza Kikosi chake cha mwisho cha Wachezaji 22 wa Fainali za Kombe la Dunia.
Mpigapicha huyo alipondwa na Gari la Maradona alipokuwa akiingia nalo ndani ya Viwanja vya Mazoezi vya Chama cha Soka cha Argentina Mjini Buenos Aires, Argentina.
Mara baada ya kumuunda Mpigapicha huyo, Maradona akamtukana na kuhoji kwanini aliweka mguu wake chini ya tairi.
Mpigapicha huyo alipewa huduma ya kwanza hapohapo kisha kukimbizwa Hospitalini.
Grant atimka Pompey
Avram Grant ameachia ngazi kama Meneja wa Portsmouth na kuna tetesi huenda akatua West Ham.
Ingawa Portsmouth imeshushwa Daraja toka Ligi Kuu kwa kumaliza ikiwa mkiani Msimu uliokwisha Mei 9, Grant aliipeleka Timu hiyo, iliyokumbwa na balaa kubwa la kifedha na hata kunusurika kuwa mufilisi na kuwekwa chini ya Msimamizi maalum, Fainali za Kombe la FA na kutolewa kwa mbinde na Mabingwa wa England, Chelsea, kwa bao 1-0 Mei 15.
Grant alichukuwa wadhifa wa Meneja toka kwa Paul Hart Novemba mwaka jana lakini Klabu ikaingia kipindi kigumu cha fedha na mwishowe kupokwa pointi 9 na Wasimamizi wa Ligi Kuu kwa kuwekwa chini ya Msimamizi maalum ili kuinusuru isifilisiwe.
Grant ametoa shukrani zake za dhati kwa Mashabiki wa Pompey na amesema Klabu hiyo ilimfanya ajisikia nyumbani wakati yuko mbali na kwao Uyahudi.
Grant alisema: “Siwezi kulipa imani na fadhila za Mashabiki, Wachezaji na Wafanyakazi wa Pompey! Nawashukuru sana kwa kunipa nafasi na heshima ya kuwa sehemu ya Mji wenu spesheli na Klabu hii iliyotukuka!”

No comments:

Powered By Blogger