Sunday 16 May 2010

SERIE A: Inter Milan Bingwa!!
Jose Mourinho leo ameiongoza Timu yake Inter Milan kutwaa Kombe kubwa la pili Msimu huu, la kwanza likiwa Coppa Italia wiki iliyokwisha, na leo wameutwaa Ubingwa baada ya kuifunga Siena bao 1-0 kwa bao la dakika ya 57 Mfungaji akiwa Diego Alberto Milito.
Jumamosi ijayo Inter wanaweza kutwaa Kombe la 3 wakiifunga Bayern Munich kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI inayochezwa huko Madrid, Spain Uwanja wa Real Madrid, Santiago Bernabeau.
Wapinzani wao wa karibu kwenye SERIE A, AS Roma, wameifunga Chievo Verona bao 2-0 na hivyo kushika nafasi ya 2.
MATOKE0 MECHIZA LEO:
Parma 4 Livorno 1
Cagliari 1 Bologna 1
Catania1 Genoa 0
Chievo Verona 0 AS Roma 2 [41, Mirko Vucini & 45 Daniele De Rossi]
Siena 0 Inter Milan 1 [57, Diego Alberto Milito]
AS Bari 2 Fiorentina 0
Atalanta 1 Palermo 2
Sampdoria 1 Napoli 0
LA LIGA: Leo kindumbwendumbwe!!
Barcelona v Real Valladolid na Malaga v Real Madrid
Huko Spain, leo kuanzia saa 2 usiku saaza bongo, mechi za mwisho za La Liga zitachezwa na mechi zenye mvuto mkubwa ni zile za FC Barcelona watakapo wakaribisha Real Valladolid Uwanjani Nou Camp na ile ya ugenini ya Real Madrid wanaosafiri kwenda kucheza na Malaga ambazo ndizo zitaamua Bingwa ni nani.
Barcelona wako pointi moja mbele ya Real Madrid na wakishinda mechi yao watafanikiwa kutetea tena Ubingwa wao lakini hata wakifungwa na ikiwa Real atatoka sare Timu hizo zitalingana pointi lakini kwa sheria za Spain Barcelona atakuwa Bingwa kwa vile tu Timu hizo zilipokutana mara zote mbili kwenye Ligi Barca aliibuka Mshindi.

No comments:

Powered By Blogger