Tuesday 18 May 2010

Fabregas awambia Ze Gunners naenda Barca!
Kuna ripoti zimeibuka kwamba Nahodha wa Arsenal Cesc Fabregas leo amemjulisha Meneja wake Arsene Wenger anataka kuondoka kurudi Timu yake ya utotoni FC Barcelona.
Fabregas, ambae yuko Spain akitibiwa goti lake, inasemekana leo aliongea na simu na Wenger.
Habari za kutaka kuondoka kwa Mchezaji huyo zimepata nguvu zaidi baada ya Makamu wa Rais wa Barcelona, Rafael Yuste, kuongea na Radio Ona FM ya huko Spain na kusema kuwa Fabregas amewajulisha azma yake kuhama Arsenal.
Hata hivyo Yuste alikiri suala la Fabregas lazima likubaliwe na Klabu zao mbili ingawa alikiri mazungumzo yanaenda vizuri.
Fabregas alianza Soka lake pamoja na Lionel Messi kwenye Timu ya Vijana ya Barcelona na akahamia Arsenal Septemba 2003.
Kipa wa Man United auzwa Birmingham
Kipa wa Manchester United Ben Foster, miaka 27, leo alitegemewa kupimwa afya yake huko Birmingham ili kukamilisha uhamisho wake baada ya Man United kulikubali dau la Pauni Milioni 6.
Birmingham wamelazimika kumchukua Foster kufuatia kuondoka kwa Kipa wao namba moja Joe Hart ambae walimchukua kwa mkopo kutoka Manchester City kurudi Klabuni kwake.
Nae Foster amelazimika kuhama Man United baada ya kukosa namba ya kudumu huko Man United ambako aliuanza Msimu wa 2009/10 vizuri tu alipopata mamba kufuatia kuumia kwa Kipa namba moja Edwin van der Sar lakini akawa anafanya makosa uwanjani hasa kwenye mechi za Ligi Kuu dhidi ya Manchester City na Sunderland na alipopona Van der Sar akapigwa tena benchi na hilo limemfanya aikose namba kwenye Kikosi cha England cha Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger