Monday 17 May 2010

LA LIGA: Barca Bingwa!!
FC Barcelona waliitandika Real Valladolid bao 4-0 na kuwashusha Daraja na pia wao kutwaa Ubingwa wa Spain kwa mara ya pili mfululizo huku Wapinzani wao wa jadi, Real Madrid, wakitoka sare na Malaga kwa bao 1-1.
Barcelona waliianza mechi hii wakiwa nyumbani Nou Camp kwa mchecheto pengine wakijua ni lazima washinde ili wawe Mabingwa, walituliza boli pale Luis Prieto alipojifunga mwenyewe na kuwapa Barce bao la kwanza.
Kisha Pedro Rodriguez akapachika bao la pili na kuifanya Barca iwe 2-0 hadi mapumziko.
Kipindi cha pili, Barcelona waliongeza bao mbili kupitia Staa Lionel Messi na kuifanya iibuke na ushindi mnono wa 4-0 na Ubingwa wa La Liga.
Huko Malaga, Real Madrid walilazimishwa sare ya 1-1 ambayo iliwanusuru Malaga kushushwa Daraja na pia kufanya kibarua cha Kocha wa Real, Manuel Pellegrini, kiwe kwenye utata mkubwa.
Kabla kuanza Msimu huu uliokwisha jana, Real Madrid walitumia zaidi ya Pauni Milioni 200 kuwanunua Nyota Cristiano Ronaldo, Kaka, Karim Benzema na Xabi Alonso lakini mwishoni mwa Msimu wameambulia patupu.
Real Madrid imethibitisha watakaa chini na kuangalia nini cha kufanya.
Timu ambazo zimeporomoka Daraja kutoka La Liga ni Real Valladolid, Tenerife na Xerez.
Kombe la Mataifa Afrika kuchezwa Miaka Tasa!
CAF imethibitisha kuwa kuanzia Mwaka 2013, Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitafanyika katika Miaka isiyogawanyika ili isiwe ikichezwa Mwaka mmoja pamoja na Fainali za Kombe laDunia.
Mabadiliko haya yanamaanisha Fainali za 2012 ambazo zitachezwa kwa pamoja katika Nchi mbili, Gabon na Equtorial Guinea, zitafuatiwe na zile zitakazochezwa Libya Mwaka 2013 hii ikiwa ni baada ya miezi 12 tu badala ya kila Miaka miwili kama ilivyo kawaida na baada ya hapo Fainali nyingine zitakuwa Mwaka 2015.
CAF pia imetangaza kuwa yale Mashindano kwa Wachezaji wa Ndani ya Nchi, CHAN [Championship of African Nations], yatakuwa yakifanyikakila baada ya Miaka miwili katika miaka inayogawanyika na mbili kuanzia Fainali za Libya Mwaka 2014 na Fainali inayofuata itakuwa 2016.
Fainali za Kombe la Afrika, tangu 1968, zimekuwa zikifanyika kila Miaka miwili ingawa Mashindano ya kwanza yalifanyika Sudan 1957.

No comments:

Powered By Blogger