Saturday 15 May 2010

Drogba aipa Ze Bluzi FA CUP!
Didier Drogba ni Shujaa wa Chelsea baada ya kufunga goli muhimu na la pekee na kuwapa ushindi wa kutwaa Kombe la FA dhidi ya Portsmouth leo Uwanjani Wembley.
Ushindi huu umehitimisha Msimu Bora katika historia ya Chelsea kwani hii ni mara ya kwanza kutwaa Vikombe viwili katika Msimu mmoja.
Portsmouth wangeweza kupata bao walipopewa penalti baada ya Arunda Dindane kuangushwa na Juliano Belleti lakini Boateng akashindwa kufunga.
Ndipo, mara baada ya tukio hilo, Drogba akafunga bao kwa frikiki.
Frank Lampard angeweza kuipatia Chelsea bao la pili kwa penalti alipoangushwa na Michael Brown ndani ya boksi lakini alipopiga tuta hilo likaenda nje.

No comments:

Powered By Blogger