Thursday 13 May 2010

Ni Cardiff City au Blackpool kupanda LIGI KUU!!
Jana Cardiff City walifanikiwa kuwabwaga Leicester City licha ya kufungwa na hivyo kuingia Fainali kucheza na Blackpool hapo Mei 22 kuamua Timu ipi itaungana na Newcastle United na West Bromwich Albion kucheza Ligi Kuu Msimu ujao.
Katika mechi ya jana Cardiff City walifungwa 3-2 na Leicester City na kuifanya mechi iamuliwe kwa penalti kwa vile wao walishinda 1-0 kwenye mechi ya kwanza.
Katika mikwaju hiyo ya penalti Cardiff City walitoka kidedea kwa bao 4-3.

No comments:

Powered By Blogger