Thursday 13 May 2010

Wenger aungama Difensi mbovu
Arsene Wenger amethibitisha atamnunua Difenda kabla Msimu mpya kuanza baada ya kukiri Difensi yake ilikuwa mbovu kwenye Msimu uliomalizika hivi karibuni.
Katika Misimu mitano sasa Arsenal imeambulia patupu bila ya kutwaa Kombe lolote na hilo limemfanya akiri kuwa ingawa Fowadi yake ni nzuri lakini ni Difensi ambayo ilifungwa mabao 41 kwenye Ligi Kuu iliyomalizika Jumapili iliyopita ndio iliyo wakosesha Vikombe.
Inasemekana Masentahafu wa Fulham, Brede Hangeland na Yule wa Senegal Pape Diakhate ndio analenga kuwanunua.
Pia, haja ya kununua Madifenda imeongezeka kwa vile Sol Campbell, Mikel Silvestre na William Gallas Mikataba yao inakwisha na bado haijazungumzwa kama itaongezwa au vipi.
Fergie asifu wasaidizi wake
Sir Alex Ferguson amewasifu na kuwashukuru Wasaidizi wake wote kwa kazi njema na msaada wao mkubwa kwa Msimu wote ulioisha Jumapili iliyopita ambao Manchester United walimudu kushika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu, kutwaa Carling Cup na kufika hatua ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Ferguson alisema walikabiliwa na majeruhi kwa Wachezaji 16 wa Timu ya Kwanza na kukaa nje kwa zaidi ya Wiki 6 lakini Wasaidizi hao, wakiwemo wale wa Idara ya Matibabu, waliwahudumia vyema na kuhakikisha kila wakati wapo Wachezaji walio fiti kucheza.
Ferguson alisema: “Nasikia fahari kuwa na Wasaidizi hawa. Wale wa Matibabu walitoa huduma bora na wale Makocha walihakikisha Timu yeyote tunayoitupa Uwanjani imetayarishwa vyema!”
Kuna wakati, Difensi nzima ilikuwa majeruhi kuanzia Kipa Edwin van der Sar, Mabeki Garry Neville, Rio Ferdinand, Nemanja Vidic, Jonny Evans na Wes Brown na kubaki Beki mmoja tu, Patrice Evra, alie fiti na hivyo kulazimisha Viungo Darren Fletcher na Michael Carrick kucheza kama Masentahafu.
Sir Alex Ferguson anasaidiwa na Meneja Msaidizi Mike Phelan ambae aliwahi kuwa Mchezaji wa Man United aliponunuliwa mwaka 1989 kutoka Norwich City na alianza kazi hiyo ya Umeneja Msaidizi Septemba 2008.
Msaidizi mwingine wa Ferguson ni Kocha wa Timu ya Kwanza Rene Meulensteen kutoka Uholanzi aliechukua wadhifa huo Septemba 2008.
Timu ya Akiba, Rezevu, ipo chini ya Staa wa zamani Ole Gunnar Solksjaer.
Pichani Ferguson akiwa na Mike Phelan kulia kwake na Rene Meulensteen kushoto.

No comments:

Powered By Blogger