Thursday 13 May 2010

Atletico Bingwa!
Bao mbili toka kwa Diego Forlan zimewapa Atletico Madrid Ubingwa wa Kombe la Kwanza la EUROPA LIGI kwa kuwatoa Fulham kwa bao 2-1 katika mechi ilyoenda dakika 120 baada ya kuwa droo 1-1 katika 90 za kawaida.
Diego Forlan, Mchezaji wa zamani wa Manchester United, alifunga bao la kwanza kwa Atletico dakika ya 33 na Simon Davies akasawazisha dakika ya 37.
Ndipo katika kipindi cha pili cha nyongeza ya dakika 30, kwenye dakika ya 115, Diego Forlan akamalizia kazi nzuri ya mkwe wa Diego Maradona, Sergio Aguero, kwa kufunga bao la pili.
VIKOSI:
Atletico Madrid: De Gea, Ujfalusi, Perea, Dominguez, Antonio Lopez, Reyes, Paulo Assuncao, Raul Garcia, Simao, Forlan, Aguero.
AKIBA: Joel, Valera, Camacho, Jurado, Salvio, Juanito, Cabrera.
Fulham: Schwarzer, Baird, Hughes, Hangeland, Konchesky, Duff, Etuhu, Murphy, Davies, Gera, Zamora.
AKIBA: Zuberbuhler, Pantsil, Nevland, Riise, Dempsey, Greening, Dikgacoi.
REFA: Nicola Rizzoli (Italy)

No comments:

Powered By Blogger