Tuesday 11 May 2010

Capello atangaza Kikosi cha England cha Kombe la Dunia
Kocha wa England Fabio Capello amewatangaza Wachezaji 30 kikiwa ni Kikosi cha awali kitakachoingia kambini kujitayarisha na Fainali za Kombe la Dunia na baadae kupunguzwa hadi Wachezaji 23 watakaowasilishwa FIFA ifikapo Juni 1.
Katika majina hayo 30 yapo majina kadhaa yaliyowastukiza Wadau wakiwemo Adam Johnson na Michael Dawson , ambao hawajahi kuichezea England.
Pia yumo Beki Mkongwe wa Liverpool, Jamie Carragher, aliestaafu kuichezea England na Beki wa Tottenham, Ledley King, ambae huwa hawezi kucheza mechi mfululizo kwa kuwa ana matatatizo kwenye goti.
England itapiga Kambi ya mazoezi huko Austria ambako itakwenda Jumamosi na wanategemewa kucheza mechi mbili za kujipima nguvu, moja ikiwa Mei 24 watakapocheza na Mexico Uwanjani Wembley na nyingine na Japan itakayochezwa huko Graz, Austria.
MAKIPA: Joe Hart, David James, Robert Green.
WALINZI: Leighton Baines, Jamie Carragher, Ashley Cole, Michael Dawson, Rio Ferdinand, Glen Johnson, Ledley King, John Terry, Matthew Upson, Stephen Warnock.
VIUNGO: Gareth Barry, Michael Carrick, Joe Cole, Steven Gerrard, Tom Huddlestone, Adam Johnson, Frank Lampard, Aaron Lennon, James Milner, Scott Parker, Theo Walcott, Shaun Wright-Phillips.
MAFOWADI: Darren Bent, Peter Crouch, Jermain Defoe, Emile Heskey, Wayne Rooney.
Zola afukuzwa West Ham
West Ham imemtimua kazi ya Umeneja Gianfranco Zola baada ya kuitumikia Klabu hiyo tangu Septemba, 2008 alipochukua wadhifa huo kutoka kwa Alan Curbishley.
Katika Msimu wake wa kwanza na West Ham Zola aliweza kuifanya Timu hiyo imalize ikiwa nafasi ya 9 lakini Msimu huu wamefanya vibaya na kumaliza nafasi ya 17 wakiwa pointi 5 tu na nafasi moja tu juu ya Timu 3 za mkiani zilizoshushwa Daraja.
Mpaka sasa haijajulikana nani atachukua nafasi ya Zola ingawa wanatajwa kina Slaven Bilic, Kocha wa Croatia aliewahi kuichezea West Ham hapo nyuma, Bosi wa Portsmouth, Avram Grant na Kocha wa zamani wa Manchester City, Mark Hughes.
Zola amekuwa hana uhusiano mzuri na Wamiliki wapya wa West Ham, David Gold na David Sullivan, walioitwaa Klabu hiyo Januari mwaka huu.

No comments:

Powered By Blogger