Monday 10 May 2010

Ancelotti: ‘Kuifunga Man United kulitupa Ubingwa!’
Carlo Ancelotti amesema kuifunga Manchester United mara mbili kwenye Ligi Kuu Msimu huu ndio kumewapa Ubingwa ingawa kambi ya Man United bado inaamini mechi zote hizo mbili Chelsea walishinda kwa kubebwa na Marefa.
Chelsea imemaliza Msimu ikiwa pointi moja mbele ya Manchester United na kunyakua Ubingwa kwa mara ya kwanza tangu 2006.
Ingawa Chelsea inasemwa ina Wachezaji ‘Wazee’, Ancelotti amesema: “Hii Klabu inayo hatima nzuri muda ujao kwa sababu Wachezaji wetu si wazee!”
Evra ajuta!
Beki wa Manchester United Patrice Evra amebeba mzigo mkubwa wa majuto wa kuukosa Ubingwa baada ya Chelsea kuubeba hapo jana walipoitandika Wigan 8-0.
Evra ametamka: “Siku zote nimesema tusipochukua Ubingwa nakuwa nimeiangusha Man United! Hii ni mara ya kwanza sijachukua Ubingwa! Ndio kuwa wa pili ni nzuri lakini si stahili yetu!”
Evra ndie Mchezaji aliecheza mechi nyingi Manchester United Msimu huu kwa kucheza mechi 51.

No comments:

Powered By Blogger