Tuesday 11 May 2010

Ronaldinho, Adriano nje Brazil!!
Dunga, Kocha wa Brazil, hakuwaita Wachezaji Ronaldinho na Adriano kwenye Kikosi chake cha Fainali za Kombe la Dunia alipoitaja Timu yake ambayo haikuleta maajabu yeyote kwa Wadau kwani amechukua Wachezaji walewale waliokuwa wakitegemewa.
Kikosi kamili:
MAKIPA: Julio Cesar (Inter Milan), Doni (AS Roma), Gomes (Tottenham Hotspur)
MABEKI: Maicon (Inter Milan), Daniel Alves (Barcelona), Michel Bastos (Olympique Lyon), Gilberto (Cruzeiro), Lucio (Inter Milan), Juan (AS Roma), Luisao (Benfica), Thiago Silva (AC Milan)
VIUNGO: Gilberto Silva (Panathinaikos), Felipe Melo (Fiorentina), Ramires (Benfica), Elano (Galatasaray), Kaka (Real Madrid), Julio Baptista (Roma), Kleberson (Flamengo), Josue (VfL Wolfsburg).
MASTRAIKA: Robinho (Santos), Luis Fabiano (Sevilla), Nilmar (Villarreal), Grafite (VfL Wolfsburg).
Fabio amrudisha kundini Carragher lakini Scholes agoma!!
Kocha wa England, Fabio Capello, leo ametoboa kuwa alijaribu kumshawishi Kiungo wa Manchester United Paul Scholes ili arudi tena kuichezea England aliyoistaafu mwaka 2004 lakini hakufanikiwa.
Capello alisema: "Ndio niliongea nae lakini akajibu hapana! Anapendelea zaidi kuwa na Familia yake! Lakini nilijaribu kumshawishi.”
Hata hivyo, Capello amefanikiwa kumrudisha kwenye Timu ya England Beki wa Liverpool, Jamie Carragher, aliestaafu mwaka 2007.

No comments:

Powered By Blogger