Sunday 9 May 2010

KWINGINEKO ULAYA:
BUNDESLIGA: Bayern Munich Bingwa!!
Jana, rasmi Bayern Munich walitwaa Ubingwa wa Ujerumani walipoifunga ugenini Hertha Berlin, ambayo tayari ishashuka Daraja, kwa bao 3-1.
Huu ni Ubingwa wa 22 kwa Bayern Munich.
LA LIGA: Mgoma mgumu hadi Wikiendi ijayo!!
Huko Spain, Bingwa bado hajapatikana na atajulikana wikiendi ijayo kwenye mechi za mwisho za La Liga baada ya wagombea Ubingwa wawili, Real Madrid na Barcelona, kushinda mechi zao za jana.
Barcelona waliipiga Sevilla 3-2 na walimaliza mechi hiyo kwa hekaheka licha ya kuongoza kwa bao 3-0, kwa bao za Messi, Bojan na Pedrito, kwani Sevilla walipata bao mbili kupitia Kanoute na Luis Fabiano na kuufanya mwisho uwe mshikemshike.
Huko Santiago Bernabeau, Real Madrid waliishinda Athletic Bilbao 5-1 na kuwafanya wawe pointi moja nyuma ya Barcelona.
Real walipata bao la kwanza kwa penlti iliyomfanya Amorebieta wa Bilbao atolewe kwa Kadi Nyekundu na Cristiano Ronaldo kufunga.
Bilbao walisawazisha kupitia Yeste lakini kipindi cha pili Real waliangusha mvua ya magoli kupitia Gonzalo Higuain, Sergio Ramos, Karim Benzema na Marcello.
Mechi za mwisho, Barcelona wako nyumbani kuikaribisha Real Vallodolid na Real Madrid watakuwa ugenini kuikwaa Malaga.

No comments:

Powered By Blogger