Friday 14 May 2010

FAINALI: Kesho Portsmouth v Chelsea
Jumamosi, Mei 15
Wembley Stadium, Saa 11 jioni, bongo taimu
HISTORIA:
Hii ni Fainali ya 129 ya Kombe la FA na hii ni mara ya kwanza kwa Chelsea na Portsmouth kukutana kwenye hatua hii ya Fainali ingawa zimewahi kucheza mara 3 kwenye hatua za awali za Kombe hili na kila Timu ilishinda mara moja na sare moja.
Chelsea ndio Mabingwa wa Ligi Kuu Msimu huu na Portsmouth ndio Timu iliyoshika mkia na hivi kuporomoshwa kucheza Daraja la chini Msimu ujao.
Portsmouth hawajahi kuwafunga Chelsea katika mechi zao 27 za mwisho walizocheza na mara ya mwisho kuwafunga Chelsea ilikuwa Desemba1960 Portsmouth waliposhinda 1-0.
Katika mechi hizo 27 tangu Portsmouth washinde, Chelsea wameshinda mechi 21 na sare 6.
Msimu huu kwenye Ligi Kuu, Chelsea waliibamiza Portsmouth bao 5-0 huko Fratton Park na kushinda mechi ya pili 2-0 Uwanjani Stamford Bridge.
Hii ni Fainali ya 10 kwa Chelsea na wameshinda 5 na kufungwa 4.
Kwa Portsmouth, itakuwa ni Fainali yao ya 5 na wameshinda mbili, mwaka 2008 walipoitoa Cardiff City na mwaka 1939 walipoibwaga Wolves, na zile walizopoteza ni mbili za mwaka 1934 walipocheza na Manchester City na mwaka 1929 walipoivaa Bolton.
Timu zote hizi Jezi zao za kawaida ni Bluu hivyo imeamuliwa kwenye Fainali ya kesho Chelsea watavaa Jezi za Bluu, juu na chini, na stokingi nyeupe na Portsmouth watavaa juu nyeupe na chini, bukta na stokingi, rangi ya kahawia.
NINI WANASEMA:
-Mchezaji wa Portsmouth, Tal Ben-Haim: “Sijapata kuona Mashabiki kama hawa ambao hata mkifungwa na kucheza vibaya na mabaya yote yaliyotukuta Msimu huu lakini wao wameendelea kuja kutushangilia! Kama tutaweza kuwafurahisha hiyo ni zawadi tosha kwao!”
-Nahodha wa Chelsea John Terry: “Hakuna kitu kitafuta majonzi yetu ya kufungwa Moscow na Man United na wao kutwaa UEFA CHAMPIONS LIGI labda tufanikiwe kutwaa Kombe hilo la Ulaya! Lakini tuna nafasi ya kuweka historia katika Historia ya Klabu hii kwa kutwaa Vikombe viwili Msimu mmoja-kile cha Ubingwa Ligi Kuu na FA Cup!”
VIKOSI VINAVYOTEGEMEWA:
Chelsea (Fomesheni, 4-3-3): Cech; Ivanovic, Alex, Terry, A Cole; Kalou, Ballack, Lampard; Malouda, Drogba, Anelka.
Portsmouth (Fomesheni, 4-5-1): James; Finnan, Mokoena, Rocha, Mullins; Boateng, Brown, Hughes Yebda, Dindane; Piquionne
Refa: Chris Foy
Marefa Wasaidizi: John Flynn na Shaun Procter-Green
Refa wa Akiba: Andre Marrrine
NJIA WALIYOFIKA FAINALI:
Chelsea
Raundi ya 3: Chelsea 5 Watford 0
Raundi ya 4: Preston 0 Chelsea 2
Raundi ya 5: Chelsea 4 Cardiff 1
Raundi ya 6: Chelsea 2 Stoke 0
Nusu Fainali: Aston Villa 0 Chelsea 3
Portsmouth
Raundi ya 3: Portsmouth 1 Coventry 1
Marudio Raundi ya 3: Coventry 1 Portsmouth 2 (Baada ya dakika 30 za nyongeza)
Raundi ya 4: Portsmouth 2 Sunderland 1
Raundi ya 5: Southampton 1 Portsmouth 4
Raundi ya 6: Portsmouth 2 Birmingham 0
Nusu Fainali: Portsmouth 2 Tottenham 0
WAFUNGAJI KOMBE LA FA:
Chelsea: Sturridge 4, Lampard 3, Malouda 2, Drogba 2, Anelka 1, Ballack 1, Kalou 1, Terry 1, Goli la kujifunga wenyewe 1.
Portsmouth: Piquionne 3, Boateng 2, Utaka 2, Belhadj 1, Dindane 1, Mokoena 1, O'Hara 1, Owusu-Abeyie 1, Goli la kujifunga wenyewe 1.

No comments:

Powered By Blogger