Friday 14 May 2010

FIFA kupokea Maombi ya Uenyeji Kombe la Dunia 2018 & 2022 leo!!
  • 2018 WAOMBAJI: Australia, England, Ubelgiji na Uholanzi [Ubelgiji na Uholanzi zitaendesha Fainali kwa pamoja] Urusi, Spain na Ureno [Spain na Ureno zitaendesha Fainali kwa pamoja], USA [pia wameomba 2022].
  • 2022 WAOMBAJI: Japan, Korea ya Kusini, USA na Qatar.
Leo FIFA itapokea rasmi maombi ya Waombaji wa kuwa Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2018 na 2022.
Fainali za mwaka 2014 tayari wameshapewa Brazil.
Fainali za 2010 zitaanza huko Afrika Kusini kuanzia Juni 11 hadi Julai 11.
Maombi ya England yatawasilishwa Makao Makuu ya FIFA huko Zurich, Uswisi na Supastaa David Beckham huku akibeba Buku lenye kurasa 1752 likichambua Maombi ya England.
Beckham amesema: “Tuna Viwanja vizuri, Viwanja vya Mazoezi bora, Usafiri na Mahoteli ya uhakika!”
Kila Nchi Mwombaji imetakiwa kuwasilisha Maombi yao yakichambua Miji na Viwanja vitakavyochezwa mechi, Miundombinu na Makaridio ya gharama za uendeshaji na mategemeo ya mapato.
Baada ya FIFA kupokea Maombi hayo watayachambua na kisha Wakaguzi watatembelea kila Nchi na kuwasilisha Ripoti zao kwa Kamati Kuu ya FIFA yenye Watu 24 ambayo ndio itaamua nani atakuwa Mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 na 2022.
Uamuzi huo unategemewa kutolewa Desemba 2, 2010.

No comments:

Powered By Blogger