Sunday 9 May 2010

BINGWA NANI??????

Leo saa 12 jioni, saa za Bongo, Timu zote 20 za Ligi Kuu zitaingia Viwanja mbalimbali kucheza mechi zao za mwisho za Ligi Kuu Msimu wa 2009/10 lakini ni mechi mbili tu ndizo zenye msisimko mkubwa kwa vile zitaamua Bingwa nani.
=============================
RATIBA:
Jumapili, 9 Mei 2010
[saa 12 jioni]
Arsenal v Fulham
Aston Villa v Blackburn
Bolton v Birmingham
Burnley v Tottenham
Chelsea v Wigan
Everton v Portsmouth
Hull v Liverpool
Man United v Stoke
West Ham v Man City
Wolves v Sunderland
========================
Chelsea wakiwa pointi moja mbele ya Mabingwa Watetezi Manchester United watakuwa Mabingwa wapya leo wakiifunga Wigan Uwanjani Stamford Bridge na huu utakuwa ni Ubingwa wao wa kwanza tangu 2006.
Lakini Chelsea wakijikwaa tu na kutoka sare au kufungwa na Wigan na Manchester United wakiifunga Stoke City huko Old Trafford, Man United watakuwa Mabingwa kwa mara ya 4 mfululizo, ikiwa ni rekodi, na pia kwa mara ya 19, ikiwa pia ni rekodi ambayo sasa inashikiliwa na wao na Liverpool kwa pamoja kwa vile kila Klabu imchukua Ubingwa mara 18
Arsenal wataitwaa nafasi ya 3 wakiifunga Fulham huko Emirates lakini wakiteleza tu na Tottenham kuifunga Burnley basi Tottenham wataitwaa nafasi ya 3 na hii inamaanisha wataingia moja kwa moja hatua za makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Timu inayoshika nafasi ya 4 inacheza pia UEFA CHAMPIONS LIGI lakini inaanza hatua za awali za Mchujo.
Wakati Bosi wa Chelsea Carlo Ancelotti amewaonya Wachezaji wake kutulia na kutokuwa na hofu, Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema ni upuuzi kutegemea msaada wa Chelsea ingawa ana mategemeo makubwa Wigan watajitahidi.
Wigan iliitandika Chelsea bao 3-1 katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu na Bosi wa Wigan Roberto Martinez amesema wao watacheza Soka bora ili kulinda heshima ya Soka.
Ingawa wengi wanahisi mbali ya kitimtim cha nani Bingwa, Timu nyingine hazina kitu wanachogombea kwa vile pia Timu 4 za juu zitakazocheza UEFA CHAMPIONS LIGI [Chelsea, Man United, Arsenal na Tottenham] na zile zilizoshushwa [Hull City, Burnley na Portsmouth] tayari zishajulikana, lakini ukweli ni kuwa Timu ikipanda nafasi katika msimamo wa Ligi pia inajiongezea pato la Pauni 800,000 kwa kila nafasi nah ii ni sababu tosha kwa Timu kujikakamua leo.
MSIMAMO LIGI KUU:
[Kila Timu imecheza Mechi 37 na kubakisha moja]
1. Chelsea pointi 83===  KUCHEZA UEFA CHAMPIONS LIGI
2. Man United pointi 82=KUCHEZA UEFA CHAMPIONS LIGI
3. Arsenal pointi 72===  KUCHEZA UEFA CHAMPIONS LIGI
4. Tottenham 70=====  KUCHEZA UEFA CHAMPIONS LIGI
--------------------------------------
5. Man City 66====EUROPA LIGI
6. Aston Villa 64==  EUROPA LIGI
7. Liverpool 62===  EUROPA LIGI
----------------------------------------------------
8. Everton 58
9. Birmingham 50
10.Stoke City 47
11.Blackburn 47
12.Fulham 46
13.Sunderland 44
14.Bolton 36
15.Wigan 36
16.Wolves 35
17.West Ham 34
----------------------------------------------------
18.Hull 29======= IMESHUSHWA DARAJA
19.Burnley 27==== IMESHUSHWA DARAJA
20.Portsmouth 19 = IMESHUSHWA DARAJA

No comments:

Powered By Blogger