Thursday 13 May 2010

FIFA yatangaza Wachezaji wa Timu zote Kombe la Dunia
FIFA imetoa majina ya Vikosi vya Awali vyaWachezaji 30 wa Nchi mbalimbali zitakazoshiriki Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa huko Afrika Kusini kuanzia Juni 11 hadi Julai 11.
Kila Nchi inatakiwa iwasilishe Listi yao mwisho ya Wachezaji 23 hapo Juni 1.
Kuna baadhi ya Nchi hazikupeleka namba kamili ya Wachezaji 30 ya Vikosi vyao vya awali kama vile Ujerumani yenye Wachezaji 27, Mexico na Uruguay 26, Slovakia 29.
Lakini, Korea ya Kaskazini wao tayari washapeleka Kikosi chao cha mwisho cha Wachezaji 23.
Katika majina hayo yaliyopokelewa FIFA, Wachezaji Chipukizi kabisa ni Vincent Aboubakar wa Cameroun, Christian Eriksen wa Denmark na Nassim Ben Khalifa wa Uswisi na wote wana umri wa miaka18.
Wachezaji ‘Vinjeba’ ni Makipa wa Holland Sander Boschker na David James wa England na wote wana miaka 39.
Katika majina hayo huko FIFA, Wachezaji 139 wanacheza Soka lao England, 93 Italia, 94 Ujerumani, 74 Spain na 12 Scotland.
LISTI KAMILI YA FIFA BOFYA HAPA

No comments:

Powered By Blogger