Friday 14 May 2010

Kipa wa Man United njiani kwenda Birmingham
Birmingham wako mbioni kumsaini Kipa wa Akiba wa Manchester United Ben Foster na inasemekana Klabu hizo mbili zishakubaliana kuhusu uhamisho huo na kilichobaki ni Kipa huyo kukubaliana maslahi yake binafsi na Birmingham.
Birmingham wamelazimika kutafuta Kipa baada ya Kipa wao Nambari wani, Joe Hart, ambae alikuwa hapo kwa mkopo kutoka Manchester City, kumaliza Mkataba wa huo mkopo uliodumu hadi mwishoni mwa Msimu uliokwisha Jumapili iliyopita na hivyo kutakiwa kurudi Man City.
Ben Foster amekuwa akitaka kuondoka Man United kwa kukosa namba ya kudumu hapo na hilo limesababisha hata asichukuliwe Kikosi cha England cha Kombe la Dunia ingawa kawaida alikuwemo Kikosi cha England na badala yake amechukuliwa Joe Hart.
Wakala wa Foster, Lee Payne, amethibitisha kuwa wapo kwenye hatua za mwisho za majadiliano na Birmingham.

No comments:

Powered By Blogger