Tuesday 11 May 2010

KESHO FAINALI: Fulham v Atletico Madrid
Uwanja wa HSH Nordbank Arena, Hamburg, Ujerumani
SAA 3 DAKIKA 45 USIKU [Bongo Taimu]


NJIA YA FAINALI KWA FULHAM
Kundi E
Fulham walianza Kundi hili kwa sare ya 1-1 na PFC CSKA Sofia na kisha kushinda 1-0 dhidi ya FC Basel.
Mechi iliyofuata AS Roma walifunga bao dakika za majeruhi na kufanya Fulham 1 AS Roma 1 lakini katika marudiano ya Timu hizi AS Roma ilitoka kidedea.
katika mechi iliyofuata Fulham waliibwaga CSKA bao 1-0 na ilibidi washinde mechi yao ya mwisho ya Kundi hili ili wasonge mbele na walimudu kuifunga FC Basel 3-2.
Raundi ya Timu 32
Fulham v FC Shakhtar Donetsk [Jumla ya Mabao 3-2]
Fulham walishinda mechi ya kwanza 2-1 na marudio ilikuwa sare 1-1.
Raundi ya Timu 16
Fulham v Juventus [Jumla ya Mabao 5-4]
Katika mechi ya kwanza huko Turin, Fulham walichapwa 3-1 na Juventus na kwenye mechi ya marudiano Uwanjani Craven Cottage, Fulham walijikuta wako nyuma kwa bao la David Trezeguet na kila mtu alijua Fulham wako nje.
Lakini, Juventus wakapata pigo pale Nahodha wao Fabio Cannavaro alipotolewa nje kwa Kadi Nyekundu na mabao kutoka kwa Bobby Zamora, Gera, bao mbili, na Clint Dempsey yaliwapa ushindi mnono wa bao 4-1 na kusonga mbele.
Robo Fainali
Fulham v VfL Wolfsburg [Jumla ya Mabao 3-1]
Fulham walishinda mechi zote mbili kwa bao 2-1 na 1-0 na walikuwa Mastraika wa Fulham, Damien Duff na Bobby Zamora, ndio Mashujaa kwa kufunga mabao hasa katika mechi ya pili ugenini Uwanjani VfL Wolfsburg Arena pale Bobby Zamora alipopachika bao pekee na la ushindi sekunde 25 tu tangu mechi ianze.
Nusu Fainali
Fulham v Hamburg [Jumla ya Mabao 2-1]
Uwanja wa Hamburg ndio ulipangwa kufanywa Fainali ya EUROPA LIGI, Uwanja wa HSH Nordbank Arena, na Wadau walitegemea Hamburg watajitutumua ili kucheza Fainali ‘homu graundi’ na kutwaa Kombe kilaini.
Lakini, Fulham walimudu kutoka sare 0-0 hapo Allianz Arena na kuitwanga Hamburg 2-1 huko Craven Cottage kwa bao za Simon Davies na Gera.
NJIA YA FAINALI KWA ATLETICO MADRID
UEFA CHAMPIONS LIGI Kundi D
Atletico Madrid walianzia kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI wakiwa Kundi moja na APOEL, FC Porto na Chelsea lakini walimaliza Kundi hili wakiwa nafasi ya 3 na kutupwa nje na kuchomekwa kwenye EUROPA LIGI.
Raundi ya Timu 32
Atletico Madrid v Galatasaray [Jumla ya Mabao 3-2]
Atletico walitoka sare na Galatasaray Uwanjani kwao Vicente Calderon ya 1-1 lakini katika mechi ya marudiano huko Uturuki, Diego Forlan alifunga bao la pili na la ushindi dakika ya 90 na kuwapa Atletico ushindi wa 2-1.
Raundi ya Timu 16
Atletico Madrid v Sporting Lisbon [Jumla ya Mabao 2-2, Atletico wasonga kwa mabao ya ugenini]
Baada ya sare ya 0-0 nyumbani, Sporting Lisbon na Atletico Madrid zilitoka sare 2-2 huko Ureno na kuifanya Atletico isonge kwa bao za ugenini.
Robo Fainali
Atletico Madrid v Valencia [Jumla ya Mabao 2-2, Atletico wasonga kwa mabao ya ugenini]
Kwa mara nyingine tena, Atletico Madrid walinufaika kwa mabao ya ugenini baada ya suluhu ya 0-0 nyumbani na 2-2 ugenini.
Nusu Fainali
Atletico Madrid v Liverpool [Jumla ya Mabao 2-2, Atletico wasonga kwa mabao ya ugenini]
Diego Forlan alifunga bao na kuwapa ushindi Atletico wa bao 1-0 dhidi ya Liverpool na katika marudiano huko Anfield, Liverpool walishinda 2-1.
Huko Anfield, Liverpool walipata bao kupitia Alberto Aquilani na kufanya ngoma iende dakika 30 za nyongeza na katika kipindi hicho Yossi Benayoun aliifungia Liverpool bao la pili lakini alikuwa Diego Forlan tena aliefunga bao moja na kuiwezesha, kwa mara nyingine tena, Atletico isonge kwa bao la ugenini.

No comments:

Powered By Blogger