Wednesday 12 May 2010

McClaren Bosi mpya Wolfsburg
Kocha wa zamani wa England Steve McClaren amesaini Mkataba wa miaka miwili na Klabu ya Ujerumani VfL Wolfsburg mara tu baada ya kuiwezesha Klabu ya Uholanzi FC Twente kutwaa Ubingwa wa Uholanzi Msimu huu kwa mara ya kwanza katika miaka 45 ya historia yao.
McClaren, miaka 49, alitimuliwa kama Kocha wa England mwaka 2007 aliposhindwa kuipeleka England Fainali za EURO 2008.
Wolfsburg ndio walikuwa Mabingwa wa Ujerumani mwaka 2009 .
McClaren alikuwa Meneja Msaidizi huko Derby County na Manchester United, chini ya Sir Alex Ferguson, na kisha kuhamia Middlesbrough kama Meneja kamili na kuifanya Klabu hiyo inyakue Carling Cup mwaka 2004 na kuipeleka Fainali ya UEFA Cup mwaka 2006.
Alichaguliwa kama mrithi wa Kocha wa England, Sven-Goran Eriksson, Agosti 2006.
Rufaa ya Ribery yapangiwa tarehe
Fowadi wa Bayern Munich, Franck Ribery, atajua siku 4 kabla ya Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI kama ataweza kucheza Fainali hiyo itakayochezwa Mei 22 huko Santiago Bernabeau kati ya Timu yake, Bayern, na Inter Milan wakati CAS, Mahakama ya Usuluhishi Michezoni itakapokaa kujadili rufaa yake ya kufungiwa mechi 3 na UEFA itakaposikilizwa.
Ribery alitolewa kwa Kadi Nyekundu katika mechi ya Nusu Fainali na Lyon alipomchezea rafu Lisandro Lopez na baadae UEFA ikamwongezea adhabu kwa kumfungia mechi 3.
Bayern wakakata rufaa kwa UEFA ambao waliitupilia mbali rufaa hiyo na ndipo Bayern wakaamua kukata rufaa CAS ambao waitajadili na kutoa uamuzi Mei 18.

No comments:

Powered By Blogger