Friday 14 May 2010

CAF yathibitisha Togo huru
CAF leo imetangaza rasmi kuifungulia Togo toka kifungo chake cha kutocheza Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya mwaka 2012 na 2014 kufuatia kujitoa Fainali za mashindano kama hayo yaliyofanyika Nchini Angola mwezi Januari baada ya Basi lao kushambuli kwa risasi na Waasi wa Jimbo la Angola la Cabinda na kumuua Dereva wa Basi hilo pamoja na Maafisa wawili wa Togo.
Kufunguliwa kwa Togo kunafuatia usuluhishi wa Sepp Blatter, Rais wa FIFA, ambae aliombwa na CAS [Court of Arbitration for Sports], Mahakama ya Usuluhisho kwa Michezo, kusuluhisha baada ya Togo kukata rufaa kwao.
Leo, CAF, baada ya Kikao cha Kamati Kuu yao huko Cairo, Misri, imetangaza rasmi kufunguliwa kwa Togo na kuthibitisha Togo watashirikishwa kwenye Mchujo wa kuingia Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika za Mwaka 2012 zitakazofanyika Nchini Gabon na Equtorial Guinea kwa pamoja.

No comments:

Powered By Blogger