Wednesday 12 May 2010

Blackpool Fainali kuingia LIGI KUU
Blackpool, wakiwa ugenini Uwanja wa City, katika mechi ya marudiano, waliweza kuwafunga wenyeji wao Nottingham Forest bao 4-3 na kutinga Fainali ya kupata Timu moja itakayoungana na Newcastle United na West Bromwich Albion ambazo tayari zishapanda Daraja kuingia Ligi Kuu Msimu ujao.
Kwenye mechi ya kwanza, Blackpool walishinda 2-1 na hivyo wamefuzu kuingia Fainali kwa jumla ya bao 6-4.
Hapo jana, Mabao ya Forest yalifungwa na Earnshaw, dakika ya 66,7, Adebobala, 90 na yale ya Blackpool yalifungwa na Campbell, dakika ya 56, 76 na 79, na Dobbie, 72.
Blackpool watacheza Fainali na mshindi wa mechi ya leo kati ya Cardiff City na Leicester City.
Kwenye mechi ya kwanza Cardiff City walishinda bao 1-0 ugenini.
Ufaransa yawatupa nje Viera, Nasri & Benzema
Kocha wa Ufaransa, Raymond Domenech, ametangaza Kikosi chake cha awali cha Wachezaji 30 watakaojitayarisha kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Juni 11 huko Afrika Kusini na Kikosi hicho kinabidi kipunguzwe na kuwasilishwa FIFA majina 23 tu ifikapo Juni 1.
Habari kubwa kuhusu Kikosi hicho ni kutemwa kwa Wachezaji Samir Nasri wa Arsenal, Patrick Viera wa Manchester City na Karim Benzema wa Real Madrid.
Vilevile, kivutio ni kuchaguliwa kwa Thierry Henry wa Barcelona na William Gallas wa Arsenal licha ya kuwa na Msimu wa kusuasua kwa Henry kupigwa benchi huko Barcelona kila mechi na Gallas kuwa majeruhi kwa muda mrefu.
Katika Fainali za Kombe la Dunia, Ufaransa wapo Kundi moja na Wenyeji Afrika Kusini, Mexico na Uruguay.
Kikosi kamili:
MAKIPA: Hugo Lloris (Olympique Lyon), Steve Mandanda(Olympique Marseille), Cedric Carrasso (Girondins Bordeaux), Mickael Landreau (Lille)
WALINZI: Bacary Sagna (Arsenal), Patrice Evra (Manchester United), William Gallas (Arsenal), Eric Abidal (Barcelona), Rod Fanni (Stade Rennes), Sebastien Squillaci (Sevilla), Adil Rami (Lille), Marc Planus (Girondins Bordeaux), Gael Clichy(Arsenal), Anthony Reveillere (Olympique Lyon)
VIUNGO: Lassana Diarra (Real Madrid), Alou Diarra(Girondins Bordeaux), Jeremy Toulalan (Olympique Lyon), Florent Malouda (Chelsea), Yoann Gourcuff (Girondins Bordeaux), Abou Diaby (Arsenal), Yann M'Vila (Stade Rennes)
MAFOWADI: Thierry Henry (Barcelona), Nicolas Anelka (Chelsea), Andre-Pierre Gignac (Toulouse), Franck Ribery (Bayern Munich), Sidney Govou (Olympique Lyon), Djibril Cisse (Panathinaikos), Hatem Ben Arfa (Olympique Marseille), Mathieu Valbuena (Olympique Marseille), Jimmy Briand (Stade Rennes)

No comments:

Powered By Blogger