Saturday 15 May 2010

Wigan yamchota Mchezaji wa Paraguay
Wigan imemsajili Beki wa Kimataifa wa Paraguay Antolin Alcaraz kutoka Klabu ya Ubelgiji Club Brugge na habari hizi zimethibitishwa na Meneja wa Wigan Roberto Martinez.
Alcaraz, miaka 27, amewahi kuchezea Klabu za Fiorentina ya Italia na SC Beira Mar ya Ureno.
Mchezaji huyo ambae ndie usajili wa kwanza wa Wigan kwa Msimu ujao atajiunga na Klabu yake mpya mara baada Fainali za Kombe la Dunia ambako Nchi yake Paraguay inashiriki.
Leonardo kutimka AC Milan
Bosi wa AC Milan Leonardo, ambae ni Staa wa zamani wa Brazil na alikuwemo Timu iliyotwaa Ubingwa wa Dunia 1994, ametangaza kuwa amekubaliana na Uongozi wa Klabu hiyo kuachia ngazi.
Leonardo, miaka 40, alipewa wadhifa wa Umeneja mwezi Mei mwaka jana alipoondoka Carlo Ancelotti kwenda Chelsea na kabla ya hapo alikuwa ni Mkurugenzi wa Ufundi Klabuni hapo.
Msimi huu ameiwezesha AC Milan kunyakua nafasi ya 3 ingawa Ligi inakwisha wikiendi hii kwa vile Timu ya 4, Sampdoria, wako nyuma yao kwa pointi 3 na tofauti ya magoli kwao ni kubwa mno hivyo Sampdoria hawawezi kuwashika.
Pia, AC Milan hawawezi kupanda nafasi ya pili kwa vile AS Roma wako mbele yao kwa pointi 10 na Inter Milan wako pointi 12 mbele.

No comments:

Powered By Blogger