Tuesday 11 May 2010

Hodgson wa Fulham ateuliwa Bora na Wenzake
Roy Hodgson ameshinda Tuzo ya Meneja Bora wa Mwaka iliyotolewa na Chama cha Mameneja wa Ligi [LMA=League Managers Association] kwa kuiwezesha Klabu yake Fulham ishike nafasi ya 12 kwenye Ligi Kuu England na pia kuiingiza Fainali ya EUROPA LIGI ambapo Mei 12 watacheza na Atletico Madrid huko Hamburg, Ujerumani.
Harry Redknapp wa Tottenham ndie alienyakua Tuzo ya Meneja Bora wa Ligi Kuu, tuzo inayotolewa na Wadhamini wa Ligi Kuu Barclays.
Rooney ndie Mchezaji Bora Ligi Kuu
Straika wa Manchester United na England Wayne Rooney ametunukiwa Tuzo ya Barclays ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu.
Rooney alifunga goli 26 kwenye Ligi na Tuzo hii inafuatia Tuzo za PFA [Chama cha Wachezaji Soka wa Kulipwa] na ile ya Waandishi wa Soka.
Uteuzi wa Mchezaji Bora wa Barclays hufanywa na Jopo la Viongozi wa Vyama vya Soka, Waandishi na Mashabiki.
Wakati huohuo, Fabio Capello, Meneja wa England, amesema Rooney atakuwa fiti kwa ajili ya Kambi ya Timu hiyo itakayoanza Jumamosi huko Austria.
Capello anategemewa kukitangaza Kikosi cha awali cha Wachezaji 30 watakaoingia kambini leo Jumanne.
Rooney amekuwa akikumbwa na majeruhi mwishoni mwa Msimu huu uliokwisha Jumapili ya juzi na siku hiyo, akicheza mechi ya mwisho ya Ligi Kuu ya Klabu yake Manchester United ilipoifunga Stoke City bao 4-0, alilazimika kutoka nje baada ya kusikia maumivu.
Lakini Capello ameondoa wasiwasi kwa kusema Rooney atarudi uwanjani ndani ya wiki mbili.

No comments:

Powered By Blogger