Meneja wa Tottenham Harry Redknapp amenyakua Tuzo ya kuwa Meneja Bora wa Msimu.

Redknapp alichukua hatamu Tottenham Oktoba 2008 huku Timu ikiwa mkiani kwenye Ligi Kuu na Msimu huu ipo nafasi ya 4 na inawezekana hata kuipiku Arsenal na kushika nafasi ya 3 ikiwa wataifunga Burnley na Arsenal kufungwa na Fulham siku ya Jumapili.
Redknapp amekuwa Meneja wa pili kushinda Tuzo hii tangu Ligi Kuu ianzishwe bila Timu yake kuwa Bingwa.
Meneja wa kwanza kuikwapua Tuzo bila ya kuwa Bingwa ni George Burley alietunukiwa baada ya kuiwezesha Ipswitch Town ishike nafasi ya 5 Msimu wa mwaka 2000/01.
Tuzo hii ya Meneja Bora hutolewa na Wadhamini wa Ligi Kuu, Barclays, na jopo la uteuzi huwa ni Vyama vya Soka, Vyombo vya Habari na Mashabiki.
No comments:
Post a Comment