Monday 3 May 2010

Ze Gunners yapigwa!!
Blackburn 2 Arsenal 1
Huko Ewood Park, kwenye mechi ya Ligi Kuu, Blackburn Rovers wamewafunga Arsenal kwa bao 2-1 katika mechi ya pili na ya mwisho ya Ligi kwa leo.
Arsenal ndio walikuwa wa kwanza kufunga kupitia Robin van Persie na Blackburn wakasawazisha Mfungaji akiwa David Dunn.
Bao la ushindi la Blackburn liliingizwa na Beki Chris Samba kufuatia kona.
Hiki ni kipigo cha 3 kwa Arsenal katika mechi zao nne za mwisho za Ligi lakini bado yuko nafasi ya 3.
Timu hizi zimebakisha mechi moja ili kumaliza Ligi Jumapili ijayo.

No comments:

Powered By Blogger