Saturday 8 May 2010

KWINGINEKO ULAYA:
La Liga: Barca na Real zafukuzana!!!
Huko Spain kwenye La Liga ni mbio kati ya Vigogo wawili huku Mabingwa Watetezi, Barcelona wakiongozwa na Lionel Messi, ndio wako kileleni kwa pointi moja dhidi ya Mahasimu wao wakubwa Real Madrid wanaoongozwa na Cristiano Ronaldo.
Kila Timu imebakiwa na mechi mbili na wikiendi hii Real wanacheza na Athletic Bilbao na Barca watakwaana na Sevilla.
Barcelona wanaweza kuutwaa Ubingwa wikiendi hii ikiwa watashinda na Real kutoka sare.
Serie A: Inter wanyemelea Ubingwa
Huku kila Timu zimebakiwa na mechi mbili, Inter Milan ndio wanaongoza Serie A na AS Roma ni wa pili.
Inter, wanaocheza na Chievo Verona Jumapili, wanaweza kuutwaa Ubingwa hiyo Jumapili wakishinda na AS Roma kutoka sare au kufungwa na Cagliari.
Ligue 1: Olympique MAarseille tayari Bingwa
Olympique Marseille tayari washautwaa Ubingwa wa Ligue 1 hii ikiwa ni mara yao ya kwanza baada ya miaka 18.
Bundesliga: Bayern Munich anusa Ubingwa!
Bayern Munich anaongoza Ligi akiwa pointi 3 mbele ya Schalke na ana tofauti kubwa ya magoli [goli 17] na hivyo labda itokee balaa kubwa lisiloelezeka ili aukose Ubingwa.
Bayern wako ugenini kucheza na Hertha Berlin.

No comments:

Powered By Blogger