Friday 7 May 2010

Obi kuikosa Fainali ya FA CUP
Kiungo kutoka Nigeria anaechezea Chelsea, John Mikel Obi, atazikosa mechi za mwisho za Klabu yake ikiwemo Fainali ya Kombe la FA Mei 15 na Portsmouth baada ya kufanyiwa operesheni ndogo ya goti.
Obi pia itaikosa mechi ya Chelsea Jumapili watapomaliza Ligi Kuu kwa kucheza na Wigan.
Mchezaji huyo aliumia goti Chelsea walipocheza na Bolton.
Man United kuzuru Marekani na Canada Majira ya Joto
Manchester United watacheza gemu nne huko USA na Canada katika ziara ya kabla kuanza Msimu mpya.
Man United kwanza wataenda Chicago ambako ni nyumbani kwa wadhamini wao wapya wa Jezi, AoN, hapo Julai 12 kwa mazoezi na kisha watacheza na Celtic ya Scotland Julai 16 Uwanja wa Rogers Centre huko Toronto, Canada.
Julai 21 watacheza na Philadelphia Union na Julai 25 wataivaa Kansas City Wizards.
Julai 28, Manchester United watacheza na Kombaini ya Mastaa wa Ligi ya MLS Mjini Houston.
Hii itakuwa ziara ya tatu kwa Man United Nchini Marekani baada ya kuzuru mwaka 2003 na 2004.
Man City yasisitiza Mancini kubaki!
Manchester City imetangaza haina nia ya kumtimua Meneja wake Roberto Mancini aliemrithi Mark Hughes mwezi Desemba mwaka jana baada ya kukosa nafasi ya kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao walipofungwa na Tottenham 1-0 hapo juzi.
Msimu ujao, England itawakilishwa na Chelsea, Manchester United, Arsenal na Tottenham kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI kwa vile zitamaliza Ligi Kuu zikiwa nafasi 4 za juu.
Man City imesisitiza Mancini ataendelea kuijenga Klabu hiyo na wanategemea Msimu ujao kufanya vyema zaidi chini yake.

No comments:

Powered By Blogger